• +255 755 310 367
  • info@stmonicawasa.ac.tz

MICHEZO NI AFYA

Michezo huwajenga vijana kuwa wakakamavu, wenye afya njema na wenye kufikiri sawa sawa.

ELIMU YA VITENDO NA KUJITEGEMEA

Tunawaandaa vijana kuyakabili mazingira yao kwa kufanya shughuli za mikono.

MALEZI YA KIMWILI NA KIROHO

Vijana wanaandaliwa kimwili na Roho kujenga kizazi Bora.

TUNAJENGA KIZAZI BORA

Tunamuandaa mwanafunzi kujitegemea kwa kupata stadi mbalimbali za maisha

Karibu ST. Monica Sekondari

Shule ya Sekondari St. Monica Wasa inayomilikiwa na Masista Wamisionari wa Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu- Iringa, ilianzishwa rasmi tarehe 21/03/2019. Shule ni ya bweni na inapokea wa wanafunzi wa jinsi zote yaani wakike na wakiume, bila kujali dini, kabila, rangi au tofauti yoyote ile.

St. Monica sekondari inatoa elimu ya sekondari (Ordinary Secondary Education - O'Level) yaani kuanzia kidato cha kwanza (Form I) mpaka kidato cha nne (Form IV).

Shule ina mazingira mazuri na tulivu ya kujifunzia ikiwemo madarasa ya kutosha, maabara zenye vifaa toshelevu, maktaba ya kisasa yenye vitabu vya kutosha na Walimu mahiri watakao mlea mwanao kitaaluma na kimaadili...

Soma zaidi

Kwanini Uchague ST. Monica Wasa Sekondari?

Shule ya St. Monica Wasa Sekondari imejitofautisha katika nyanja mbalimbali kwa kutoa elimu bora kwa watoto wote, kujikita katika ujenzi wa kizazi chenye kuleta manufaa kwa jamii na dunia kwa ujumla hapo baadaye. Tunagusa nyanja zote muhimu kama ifuatavyo:

ELIMU

Shule ya Sekondari St Monica Wasa ni mahali sahihi kwa ajili ya elimu bora itakayompa mwanao mwanga wa maisha.

MALEZI

Shule imejikita kutoa malezi stahiki yatakayomfanya mtoto/mwanafunzi akubalike katika jamii yote.

ELIMU YA KUJITEGEMEA

Shule inamwandaa mwanafunzi kujitegemea kwa kupata stadi mbalimbali za maisha ikiwemo ufugaji na kilimo.

09

Masomo

200

Wanafunzi

27

Waalimu & wafanyakazi

3

Maabara

Je! ungependa kujifunza zaidi kuhusu shule yetu?

Wasiliana nasi sasa...!